ARGENTINA VINARA KWA UBORA DUNIANI

Leave a Comment

 Shirikisho la Soka duniani Fifa imetoa orodha ya Ubora Duniani kwa mwezi wa Nane ambapo Argentina inaongoza ikiwa nafasi ya kwanza.
Ubelgiji wao wako katika nafasi ya pili huku mabingwa wa dunia Ujerumani wakiwa katia nafasi ya tatu.
Kwa Afrika, Nchi za juu kabisa ni zile zile na zimeshika Nafasi hizo hizo za Mwezi uliopita na hizo ni Algeria ambao wako Nafasi ya 19 wakifuaťiwa na Ivory Coast ambao ni wa 21.
Kwa nchi za ukanda wa afrika mashariki Uganda wanaongoza wakiwa nafasi ya 71,Rwanda wako nafasi ya 78, kenya wao wanashika nafasi ya 116, Burundi wao wako nafasi 134 huku Tanzania wakiwa nafasi ya 140.
Orodha ya ubora duniani
1 Argentina
2 Belgium
3 Germany
4 Colombia
5 Brazil
6 Portugal
7 Romania
8 Chile
9 Wales
10 England
Next PostNewer Post Previous PostOlder Post Home

0 comments:

Post a Comment